• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Atembelea Eneo La Mradi Wa Shule Ya Wasichana Ya Mkoa Itakapojengwa

Imewekwa Kwenye: June 28th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase (mbele) akiongoza msafara kuelekea eneo ambapo shule ya wasichana ya Mkoa itajengwa.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase leo juni 28, 2023, ametembelea eneo la kata ya Busale wilayani Kyela, ambapo mradi wa shule ya wasichana ya mkoa inatarajiwa kuanza kujengwa.

Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ameambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, wakuu wa taasisi, Idara na vitengo.

Akizungumza katika eneo la mradi, Mhe. Mkuu wa wilaya amesema, anatoa shukrani zake za dhati kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambae ameikumbuka wilaya ya Kyela na kutuletea mradi wa shilingi bilioni 4 ambapo hadi muda huu shilingi bilioni 3 tayari zipo katika akaunti tayari kwa kuanza mradi wa shule ya wasichana ya mkoa. Pia ameahidi kuto muangusha Mhe. Rais kwa kuusimamia mradi na kuukamilisha kwa wakati.

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa wilaya amewataka wataalam kuhakikisha miundombinu ya barabara inafika kwa urahisi katika eneo la mradi ikiwemo, huduma za maji na umeme ili kuukamilisha mradi kwa mda usiozidi miezi 6.

"Naomba miundo mbinu ya barabara, umeme na maji isogezwe kwa haraka katika eneo la mradi kwani fedha tunazo na tupo nyuma ya mda" amesema Mhe. Mkuu wa wilaya.

Hata hivyo amemuomba diwani wa kata ya Busale Mhe. Adam Kabeta kuwahamasisha wananchi wa kata yake, kujitokeza kwa wingi kusaidia shughuli ndogondogo katika mradi, ili kuungana na kutambua kazi kubwa inayofanywa na Mhe. Rais. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa naendeleo ya wanaKyela.

Hapa ni sehemu ya kata ya Busale wilayani Kyela ambapo mradi wa shule ya wasichana ya mkoa inatarajiwa kuanza kujengwa

Aidha amesema, ushirikiano baina ya wananchi uimarishwe ili kuwe na ulinzi shirikishi katika vifaa vya ujenzi wa mradi.

Mwisho Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ameweza kutembelea mradi wa maji Lema ili kujiridhisha na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo.

Hapa ni eneo la tenki la mradi wa maji Lema uliopo kata ya Busale.


Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa