• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Awataka Wataalam Wa Afya Kuhamasisha Wananchi Kuchukua Tahadhari Juu Ya Magonjwa Yasiyopewa Kipaumbele

Imewekwa Kwenye: February 27th, 2024

(picha kutoka Maktaba)

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase amewataka wataalam wa afya kuwahamasisha wananchi kuchukua tahadhari ili kujikinga na magonjwa yasiyo pewa kipaumbele, ikiwemo ugonjwa wa kichocho, magonjwa ya minyoo ya tumbo hasa kwa watoto chini ya umri wa miaka 15.

Mhe. Josephine Manase ameyazungumza hayo leo tarehe 26/02/2024 katika  kikao cha "PHC" kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, kikiwa na lengo la kupanga mpango mkakati wa zoezi la umezeshaji dawa za kichocho na minyoo ya tumbo shuleni. Ambapo wilaya ya Kyela inatarajia kuwafikia watoto 49769.

Aidha Mhe. Mkuu wa wilaya ya Kyela amewataka wataalam wa afya, kutoa Elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa uwepo wa choo kwa kila kaya, kwani kwa kufanya hivyo, kutapunguza kuenea kwa magonjwa.

Vilevile Mhe. Manase amewaomba wataalam hao kuwahamasisha wananchi kuwa na utaratibu ya kupima afya mara kwa mara ili kupunguza athari zitokanazo na magonjwa yasiopewa kipaumbele.

Pamoja na hayo Mhe. Manase amewasisitiza wananchi kuepuka imani potofu, kwani kuna baadhi ya jamii bado zina imani potofu ambazo hupelekea madhara makubwa katika jamii.

"Kuna jamii zinaamini kuwa mtoto akikojoa damu basi inaonekana mtoto amekua rijali yani amebaleghe ambapo jambo hilo si lakweli" Amesema Mhe. Manase.

Hata hivyo Mhe. Mkuu wa wilaya ametoa shukrani kwa Mhe. Rais na serikali ya awamu ya sita, kwa namna inavyojali wananchi hata kufanya haya mazoezi ya chanjo na umezaji dawa, ili kulinda jamii na watoto wetu dhidi ya magonjwa mbalimbali yasiyopewa kipaumbele.

Aidha amewaomba viongozi wa dini kutumia nafasi zao katika kuisaidia serikali kufikisha Elimu kwa waumini wao ili kupata jamii ambayo itafahamu kwa ukaribu magonjwa haya yasiyopewa kipaumbele na kuchukulia tahadhari.

Mwisho Mhe. Manase amesema kwa kuzingatia njia zote za kujikinga au kupiga vita magonjwa haya hususani magonjwa ya kichocho na minyoo ya tumbo wilaya ya Kyela, inaweza ikatokomeza magonjwa haya na kusiwe na maambukizi yoyote.

Kwani Serikali imetumia gharama kubwa kuhakikisha inatokomeza magonjwa haya ili wananchi wake waishi vizuri, na kutengeneza kizazi chenye afya nzuri ya mwili na akili.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO AONGOZA MCHAKATO WAKUMPATA MAKAMU MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO NA WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU

    October 01, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI ADV. FLORAH A. LUHALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MAPATO YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    September 30, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    September 22, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AFUNGA MAONESHO YA KUSINI INTERNATIONAL TRADE FAIR AND FESTIVAL YA MWAKA 2025

    September 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa