• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Azindua Ujenzi Wa Madarasa 67 Yatakayojengwa Katika Shule 21 Kwa Fedha Za UVIKO 19 Kyela

Imewekwa Kwenye: November 8th, 2021

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa, akiongea kwa uchungu juu ya wanafunzi wanaotoka kata ya Busale kwenda kusoma kijiji cha Ilima ambapo pana umbali mrefu

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa amezindua ujenzi wa madarasa 67 tarehe 08/11/2021, ujenzi utakaofanyika katika shule za sekondari 21 hapa wilayani Kyela. Akizungumza na wananchi waliojaa katika eneo la viwanja vya shule ya sekondari Busale, Mheshimiwa Mkuu wa wilaya amesema, Rais wa Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suruhu Hassan ametoa fedha itakayojenga madarasa 67 katika wilaya ya Kyela, hivyo  sisi wanaKyela yatupasa kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu kwa kujitolea kwa nguvu zote ili kuhakikisha ujenzi wa vyumba hivi vya madarasa unakamilika kwa wakati.

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ya Kyela hakusita kutoa pongezi kwa wananchi wa kata ya Busale, wakisimamiwa na diwani wao Mheshimiwa Adam Kabeta, ambae amekuwa mstari wa mbele katika kuanzisha miradi mingi ya maendeleo katika kata hiyo, na miradi yote ikiwa inatekelezwa kwa kasi kubwa. Hadi sasa kata ya Busale ina shule 2 za sekondari.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa (kuhoto), Katibu Tawala (katikati), Mheshimiwa diwani Adam Kabeta kata ya Busale(kulia) na Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Ezekiel Magehema (Nyuma) wakiwaongoza wananchi kuelekea eneo la ujenzi wa vyumba vya madarasa kufanya kazi.

Pamoja na hayo Mkuu wa wilaya ya Kyela aliwakumbusha wasimamizi wa pesa za ujenzi wa vyumba vya madarasa hayo, kuzitumia pesa hizo kadiri zilivyopangwa kutumika. Kinyume na matumizi hayo basi sheria itachukua mkondo wake. Akionesha kuguswa kwake na jinsi wananchi wa kata ya Busale wanavyojitokeza katika shughuli za maendeleo, Mkuu wa wilaya ya Kyela alitoa shilingi 50,000/= kuajili ya maji kwa mafundi waliokuwa wakiendelea na kazi ya ujenzi. Hata hivyo, Mheshimiwa Mkuu wa wilaya aliungana na wananchi hao katika shuguli za nguvu kazi.

Mkuu wa wilaya Mheshimiwa Ismail Mlawa akisaidiana kazi na wananchi wa kata ya Busale katika ujenzi wa vyumba vya madarasa

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Ndugu Ezekieli Magehema alitoa pongezi zake za dhati kwa wananchi wa kata ya Busale kwa namna wanavyoshirikiana  katika shughuli za maendeleo ya kata yao. Pia alimuhakikishia Mheshimiwa Mkuu wa wilaya kuwa atakuwa sambamba kwa kila eneo ambapo pesa hizi zinakopelekwa kwa ujenzi wa madarasa, ili kusaidia ujenzi kwenda kwa haraka na kwa tija.

Mkurugenzi Mtendaji ndugu Ezekiel Magehema akisaidiana kazi na wananchi wa kata ya Busale katika ujenzi wa vyumba vya madarasa

Mwisho mganga Mkuu wa hospitari ya wilaya Bi. Mariam Ngwere, alipata fulsa ya kutoa elimu juu ya umuhimu wa kuchanja chanjo ya UVIKO 19, ikiwa ni hiari kwa kila mwananchi kuchanja chanjo hiyo mara tu baada ya kupata elimu.

Mganga Mkuu wa Hospitari ya wilaya ya Kyela akitoa elimu juu ya chanjo ya UVIKO 19 katika uzinduzi wa ujenzi wa vyumba 67 vya madarasa katika kata ya Busale

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WA KIJIJI CHA ISANGA WAPATA FARAJA KWA KUUNGWA MKONO NA MHE. DC MANASE KWA UANZISHWAJI WA UJENZI WA ZAHANATI

    July 12, 2025
  • TSH. MILLIONI TANO (5) KUTOKA MFUKO WA ZAO LA KAKAO KUSAIDIA UANZISHWAJI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI KIJIJI CHA MPEGERE KATA YA MAKWALE

    July 10, 2025
  • WATAALAM WA AFYA KUTOKA MALAWI WAFANYA KIKAO NA WATAALAM WA AFYA KUTOKA KYELA KUJADILI NAMNA YA KUPAMBANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO

    July 02, 2025
  • BIDHAA FEKI ZILIZOINGIA KWA NJIA HARAMU ZATEKETEZWA KWA MOTO

    July 01, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa