• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mhe. Josephine Manase Aendelea Kusikiliza Kero Za Wananchi Kata Kwa Kata

Imewekwa Kwenye: October 6th, 2023


Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase amefanya ziara ya kusiliza kero za wananchi katika kata za Mikoroshini na Bondeni tarehe 05/10/2023.

Mheshimiwa Manase katika ziara yake  ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Bi. Florah A. Luhala, Katibu Tawala (W) Bi. Sabrina H. Ruhwey, Kamati ya Ulinzi na na Usalama (W), viongozi wa taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo.

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase, amezungumzia suala la barabara na kuwataka, Viongozi wa Serikali katika kata ya Mikoroshini kukaa na wananchi wa kata ya Mikoroshini ili kuwaomba wananchi wote wairuhusu Serikali ibomoe majengo yaliyojengwa katika hifadhi ya barabara ili kupisha ujenzi wa barabara mpya katika kata ya Mikoroshini.

Kuhusiana na suala la Afya Mhe Mkuu wa wilaya ya kyela amesema, kesi za malalamiko ya akina mama wajawazito zimekua nyingi, ameahidi kuzifanyia kazi kwa kukaa na watoa huduma za afya wa hospitali ya wilaya na kutatua kero za akina mama wote.

Pia amesema ataandaa mpango wa kutoa Elimu kwa akina mama kuhusiana na masuala ya uzazi ili akina mama waweze kuwa na uelewa mpana kuhusu  masuala ya Afya ya uzazi na kuepuka changamoto ya kutapeliwa na watumishi wenye tabia zisizo za kiungwana.

Pamoja na hayo Mhe. Manase amewaomba wananchi wa kata ya Mikoroshini kushirikiana katika suala la malezi ya watoto wakike ili kuepusha tabia mbovu zinazoweza kuleta madhara katika kata hiyo ikiwemo kuacha shule.

"Mtoto wa mwenzio ni wako hivyo ukimuona mtoto wa mwenzio anaenda mrama basi mrekebishe" amesema Mhe. Manase.

Akiwa katika kata ya Bondeni Mhe. Mkuu wa wilaya, amewataka wananchi wa kata ya Bondeni kukaa na kujadiliana, jinsi ya kupata eneo  la kijenga zahanati na waliwasilishe Halmashauri ili walitengee bajeti kwa utekelezaji.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Bi. Florah A Luhala amewataka wananchi wa kata ya Mikoroshini kulipa madeni ya mikopo wanayo kopa katika taasisi zinazojihusisha na kukopesha pesa ili kuepuka changamoto ya kunyang'anywa mali binafsi, ambazo huwekwa  rehani na mdaiwa.

Aidha Bi. Florah A. Luhala ameongeza kuwa Wazee wenye uhitaji maalumu waliokosa kunufaika na pesa ya TASAF, amewataka kuomba tena wakiwa na taarifa muhimu ili waweze kushughulikiwa na wataalam.

Mwisho ameahidi kuwa wahanga wote wenye sifa watafaidika na mfuko huo wa TASAF bila upendeleo wowote.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa