• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mhe. Josephine Manase Afanya Ziara Ya Kusikiliza Kero Za Wananchi

Imewekwa Kwenye: May 8th, 2023


Akizungumza na wananchi wa kata ya Nkuyu na Mababu hapa wilayani Kyela tarehe 08/05/2023, Mhesmiwa Josephine K. Manase amesema,

Ameamua kufanya ziara kwa kila kata ili kusiliza kero za wananchi, kero ambazo zinaweza kuwa ni vikwazo katika kuleta maendeleo.

Mhe. Mkuu wa wilaya ya Kyela Josephine K. Manase(katikati) akiwa anapokea mifuko 60 ya saruji, mifuko iliyotolewa na Amcos ya "Mali hai" kusaidia ujenzi wa zahanati ya Nkuyu.

Akiwa katika kusikiliza kero za wananchi wa kata ya Mababu, Mhe. Manase amesema amebaini kero kubwa 3 kutoka kwa wananchi wa Mababu, kero hizo ni kama zifuatazo;

Kukosekana kwa umeme, Barabara zisizopitika na wanufaika na Mpango wa TASAF.

Aidha akizungumzia kuhusiana na mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF), Mhe. Mkuu wa wilaya amesema tatizo kubwa ni ukosefu wa elimu kwa wananchi kwani wananchi wamewachagua baadhi ya wanufaika ambao si wahitaji kwa kiwango kikubwa.

Na amewataka wataalam kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuufahamu mpango huu wa TASAF, na kundoa changamoto hiyo katika jamii.

Kwa upande wa umeme wa REA amesema, Mkataba umesainiwa ikiwa ni phase nyingine ya kusambaza umeme kwenye vitongoji, ambapo Kyela tumepata vitongoji 98, Hivyo amewaagiza  viongozi kutoa elimu kwa wananchi wanavyongoja utekelezaji wa mradi huo, ili kuhakikisha kila mmoja anapata huduma ya umeme.

Aidha kwa upande wa  kilimo, Mhe. Manase, amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameiona kero ya wakulima kufuata "pembejeo" mbolea ya ruzuku kwa umbali mrefu, hivyo katika mwaka wa fedha ujao ameongeza vituo vya kusambaza mbolea ili kumfikia mkulima kwa urahisi zaidi.

Kata ya Mababu na Matema kwa upande wa tarafa ya Ntebela ni mojawapo ya kata ambazo zitakuwa na vituo vya kusambazia pembejeo hizo.

Pamoja na hayo, aliwaomba wananchi wa wilaya ya Kyela, kuulinda ubora wa kokoa, ili kuifanya kuwa na thamani kubwa, amewataka wananchi kutoa taarifa haraka pale wanapomuona mlanguzi analangua wakulima na kuchukua kokoa isiyo na ubora.

Kwa upande wa miundo mbinu amewataka "TARURA" kuendelea kurekebisha barabara zote hasa maeneyo yale ambayo ni muhimu kwa shughuli za wananchi.

Kwa suala la lishe mashuleni, liwe shirikishi ili wazazi wajue juu ya chakula wanachochangia ili kuondoa malalamiko ya wazazi.

Aliendelea kuwaasa wananchi wa Mababu na Kyela kwa ujmla, kuachana na mila kandamizi, hasa zile zinazomuonea mwanamke, mfano mwanamke anafukuzwa katika nyumba mara baada ya mme wake kufariki.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela ndugu Ezekiel H. Magehema akiwa kata ya Mababu, amewataka wananchi kuendelea kuchangia chakula cha watoto wao wawapo shuleni, wanafunzi waweze kupata chakula angalau kwa mulo mmoja. 

Hata hivyo ndugu Magehema, amewataka wananchi kukabiliana na ngedere, Hata kwa kutumia njia ya asili yaani kuwakamata wachache na kuwavalisha kengele ili wengine wakimbie.

Lakini pia kwa suala la mbwa wanaozagaa, amewataka wananchi kuweka mkakati wa kuwaua mbwa au kuwafungia ndani kampeni inayotakiwa kuanzia ngazi ya ubalozi.

pamoja na hayo amewasisitiza kuwa na vyoo bora, ila serikali ipo kwa ajiri ya kusimamia hayo yote kwa usaidizi wa wananchi.

Mwisho wananchi na viongozi wamepongeza ziara ya Mheshimiwa Mkuu wa wilaya kwa kuwakumbuka katika kusikiliza kero zao. ziara hii ni endelevu kwa kata zote 33 za hapa wilayani Kyela.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BIDHAA FEKI ZILIZOINGIA KWA NJIA HARAMU ZATEKETEZWA KWA MOTO

    July 01, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa