• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mradi Wa Shilingi Milioni 583 Watambulishwa wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: July 4th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule Kingamkono ameutambulisha mradi mpya wa Serikali wa ujenzi wa shule ya Sekondari yenye Gharama ya Tsh. Milioni 583 katika kata ya Muungano kijiji cha Bukinga tarehe 03/07/2024.

Katika ziara hiyo Mhe. Katule Kingamkono ameambatana na wakuu wa Idara na vitengo mbalimbali kutoka ofisi ya Mkurugenzi, ikiwemo Afisa Elimu Sekondari, Afisa Manunuzi na Mthibiti Ubora wa Majengo wa Wilaya ya Kyela.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara Uliofanyika kata ya Muungano kijiji cha Bukinga Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule Kingamkono, amewapongeza wananchi wa kijiji cha Bukinga kwa kujitoa na Kuchangia kiasi cha Tsh. Milioni 9, na kutoa eneo lenye ukubwa wa Hekali 12.7 kwaajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari katika kijiji hicho.

Aidha Mhe. Katule Kingamkono amewataka Wananchi wa kijiji cha Bukinga, kushirikiana katika kuhakikisha wanasafisha Eneo hilo kwakutoa Majani ili eneo liwe safi kwaajili ya utekelezaji wa mradi wa serikali.

Pamoja na hayo Mhe. Katule Kingamkono ametumia wasaa huo kuwakumbusha vijana kuchangamkia fursa kwani kuanzishwa kwa mradi huo kunatengeneza fursa za ajira kwa wakazi wakijiji cha bukinga na vijiji jirani.

Vilevile Mhe. Katule Kingamkono Amempongeza Mhe. diwani wa kata ya Muungano Lugano Kingdom mwambete kwa kuonesha juhudi za dhati, za kuwapambania wananchi wa kata ya Muungano mpaka juhudi hizo kuzaa matunda.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Muungano Mhe. Lugano Kingdom Mwambete, amefurahishwa sana na juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu hassan, kwa kuwasikiliza wananchi wake na kuwatekelezea mahitaji yao kwa wakati.

Pamoja na hayo, Mhe. Lugano Mwambete, Ameongeza kwa kusema; atahakikisha anasimamia mradi huo kwa ukaribu zaidi ili mradi huo uweze kumalizika kwa wakati.

Hata hivyo Bi. Eva Ngosi mkazi wa kijiji cha Bukinga kata ya Muungano ametoa shukrani nyingi kwa Serikali ya awamu ya sita, kwa kuwatatulia watoto wao adha ya kutembea umbali mrefu kwaajili ya kwenda kusoma, ambapo amesema, watoto wao wanakumbana na changamoto nyingi sana ambazo wengine zinawapelekea kuto maliza Elimu.

Mwisho Mhe. Katule Kingamkono amewataka wananchi wa kata ya Muungano, kuwa walinzi wa mali za serikali pindi miradi ya serikali inapo kuja kutekelezwa katika maeneo yao, kwani kufanya hivyo kutasaidia miradi kumalizika kwa wakati.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA MTOTO WA AFRIKA YAFANA WILAYANI KYELA

    June 16, 2025
  • VIVUTIO MBALIMBALI VINAVYOPATIKANA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA

    June 16, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA KYANGALA WALIA MACHOZI YA FURAHA BAADA YA KUPATA ZAHANATI MPYA KATIKA KIJIJI HICHO

    June 10, 2025
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA MHE. DKT. JUMA ZUBERI HOMERA AWEKA JIWE LA MSINGI SHULE YA WASICHANA KYELA COCOA GIRLS SECONDARY SCHOOL

    June 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa