• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Achangia Shilingi 500,000/= Ujenzi Wa Vyoo Shule Ya Msingi Kijila

Imewekwa Kwenye: May 13th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono, amechangia shilingi 500,000/= kwa ajiri ya ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Kijila iliyopo kata ya Nkokwa hapa wilayani Kyela.

Mchango huo ameutoa wakati akifanya mkutano wa hadhara, katika kijiji cha Kijila kata ya Nkokwa, tarehe 11/05/2023 kwa lengo la kuhamasisha ujenzi wa vyoo katika shule hiyo, Kwani vyoo vilivyopo kwa sasa si rafiki kwa matumizi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo.

Aliendelea kusema, Serikali ya awamu ya sita inawakumbuka sana wananchi wake, Hivyo kwa kupitia Halmashauri ya wilaya ya Kyela imetoa milioni 9 kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Kijila.

Aidha amewaeleza bayana wananchi wa Nkokwa kuwa, shilingi milioni 9 haiwezi kukamilisha ujenzi wa vyoo hivyo kwa wanafunzi jinsia ya kike na kiume, hivyo wananchi wa Kijila wanapaswa kuchangia mradi wa ujenzi huo.

Aidha aliwashauri wananchi kukaa kwa pamoja na kuchangia nguvu kazi hata fedha kidogo ili  kumalizia ujenzi wa vyoo hivyo.

Pasipokuwa na shaka, Wananchi wa kata ya Nkokwa walihamasika na kukubaliana kuchangia shilingi elfu 10 kwa kila kichwa ili kukamilisha ujenzi huo.

Nae Mhe. diwani wa kata ya Nkokwa Mhe. Hassan Mwambokela amemshukuru Mhe. mwenyekiti kwa hamasa kubwa ya ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Kijila katika kata ya Nkokwa na alichangia shilingi 200,000/= kwa ujenzi wa vyoo.

Pamoja na hayo mheshimiwa Mwenyekiti alipata fulsa ya kutembelea kata ya Ngonga na Katumbasongwe ili kuwapa pole wananchi kwa kukatika kwa mawasiliano baina ya kata hizo mbili baada ya daraja tegemezi kuvunjika.

Mwenyekiti wa halmashauri Katule G. Kingamkono (picha ya juu mwenye kofia) akiwa anaongea na baadhi ya wananchi wa kata ya Katumbasongwe na Ngonga, ambao wamepata adha ya kukatika kwa mawasiliano baada ya daraja la Nsesi kuvunjika.

Hata hivyo serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Kyela iliweza kupeleka boti kwa haraka ili kusaidia kurejesha mawasiliano baina ya kata hizo mbili kwa muda wakati taratibu za kutengeneza daraja hilo zikiendelea.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO AONGOZA MCHAKATO WAKUMPATA MAKAMU MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO NA WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU

    October 01, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI ADV. FLORAH A. LUHALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MAPATO YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    September 30, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    September 22, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AFUNGA MAONESHO YA KUSINI INTERNATIONAL TRADE FAIR AND FESTIVAL YA MWAKA 2025

    September 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa