• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Achangia Shilingi 500,000/= Ujenzi Wa Vyoo Shule Ya Msingi Kijila

Imewekwa Kwenye: May 13th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono, amechangia shilingi 500,000/= kwa ajiri ya ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Kijila iliyopo kata ya Nkokwa hapa wilayani Kyela.

Mchango huo ameutoa wakati akifanya mkutano wa hadhara, katika kijiji cha Kijila kata ya Nkokwa, tarehe 11/05/2023 kwa lengo la kuhamasisha ujenzi wa vyoo katika shule hiyo, Kwani vyoo vilivyopo kwa sasa si rafiki kwa matumizi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo.

Aliendelea kusema, Serikali ya awamu ya sita inawakumbuka sana wananchi wake, Hivyo kwa kupitia Halmashauri ya wilaya ya Kyela imetoa milioni 9 kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Kijila.

Aidha amewaeleza bayana wananchi wa Nkokwa kuwa, shilingi milioni 9 haiwezi kukamilisha ujenzi wa vyoo hivyo kwa wanafunzi jinsia ya kike na kiume, hivyo wananchi wa Kijila wanapaswa kuchangia mradi wa ujenzi huo.

Aidha aliwashauri wananchi kukaa kwa pamoja na kuchangia nguvu kazi hata fedha kidogo ili  kumalizia ujenzi wa vyoo hivyo.

Pasipokuwa na shaka, Wananchi wa kata ya Nkokwa walihamasika na kukubaliana kuchangia shilingi elfu 10 kwa kila kichwa ili kukamilisha ujenzi huo.

Nae Mhe. diwani wa kata ya Nkokwa Mhe. Hassan Mwambokela amemshukuru Mhe. mwenyekiti kwa hamasa kubwa ya ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Kijila katika kata ya Nkokwa na alichangia shilingi 200,000/= kwa ujenzi wa vyoo.

Pamoja na hayo mheshimiwa Mwenyekiti alipata fulsa ya kutembelea kata ya Ngonga na Katumbasongwe ili kuwapa pole wananchi kwa kukatika kwa mawasiliano baina ya kata hizo mbili baada ya daraja tegemezi kuvunjika.

Mwenyekiti wa halmashauri Katule G. Kingamkono (picha ya juu mwenye kofia) akiwa anaongea na baadhi ya wananchi wa kata ya Katumbasongwe na Ngonga, ambao wamepata adha ya kukatika kwa mawasiliano baada ya daraja la Nsesi kuvunjika.

Hata hivyo serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Kyela iliweza kupeleka boti kwa haraka ili kusaidia kurejesha mawasiliano baina ya kata hizo mbili kwa muda wakati taratibu za kutengeneza daraja hilo zikiendelea.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa