• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI WA CCM TAIFA AFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

Imewekwa Kwenye: February 23rd, 2025

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Taifa Ndg. Maganya Abdul Fadhil Rajab, amefanya ziara ya kukagua Miradi ya maendeleo ikiwa ni kuona kutekeleza wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) tarehe 23/02/2025.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa (Mbeya Girls) Shule ya Sekondari ya Wazazi Ngana,Jengo la Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kyela.

Ziara hiyo imeambatana na zoezi la upandaji miti katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Mbeya Girls, kama njia mojawapo ya uhifadhi na  utunzaji Mazingira.

Akiwa katika Shule ya Sekondari ya Wasichana, Ndugu. Maganya ameuagiza uongozi wa Wilaya kusimamia mradi huo na kuhakikisha majengo yaliyobaki yanakamilika kwa viwango bora na Wanafunzi wanapata masomo  katika mazingira mazuri.

Aidha  akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya wasichana Mbeya  pamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ngana kwa nyakati tofauti Ndg.Maganya amewasihi wanafunzi hao kuwa na nidhamu nzuri pamoja na kufanya juhudi katika masomo yao, kujiepusha na vishawishi vitakavyosababisha kutotimiza ndoto zao.

Aidha Ndugu. Fadhil Rajab ameupongeza Uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Kyela Kwakuwajali wazee kwakuweka Madirisha yaliyowekwa Alama kwaajili ya kuwarahisishia Wazee kufahamu mahali wanapotakiwa kutibiwa katika Vyumba vya Wazee.

Ndugu. Maganya ameongeza kuwa sehemu nyingi alikopita Vituo vya Afya vimejengwa vizuri na kuona vyumba vya matibabu kwa ajili ya wanawake na kupumzikia watoa huduma lakini hakuna vyumba vya wazee.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe. Josephine Manase amemshukuru Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi kwa ziara yake ya kukagua Miradi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela,pia amesema uongozi wa Wilaya utahakikisha unasimamia miradi kwa kufuata vigezo na viwango vilivyopangwa ili kuhakikisha Wananchi wanapata huduma stahiki.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATAALAM WA AFYA KUTOKA MALAWI WAFANYA KIKAO NA WATAALAM WA AFYA KUTOKA KYELA KUJADILI NAMNA YA KUPAMBANA NA MAGONJWA YA MLIPUKO

    July 02, 2025
  • BIDHAA FEKI ZILIZOINGIA KWA NJIA HARAMU ZATEKETEZWA KWA MOTO

    July 01, 2025
  • KYELA YAFANIKISHA UNUNUZI WA GARI JIPYA AINA YA TOYOTA HILUX KUPITIA MAPATO YA NDANI KWA TSH. MILLIONI 149.1

    June 30, 2025
  • SERIKALI YAWAPUNGUZIA WANANCHI ADHA YA ELIMU KWA KUJENGA SHULE KARIBU YAO

    June 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa