• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Namshukuru Mhe Rais Wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Kwa Kutuona Wanakijiji Wa Ikombe-Noreen Mwanjela

Imewekwa Kwenye: October 1st, 2020

Afisa tarafa wa tarafa ya Ntebela iliyopo katika wilaya ya Kyela bi. Noreen Mwanjela amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Joseph Pombe Magufuli, kwa kuwapelekea mradi wa maji Safi na salama katika kijiji cha Ikombe kilichopo katika kata ya Matema wilayani hapa. 

Akizungumza leo tarehe 1/10/2020 kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Kyela, bi. Noreen amesema; 

Leo ni siku ya kuvunja kamati ya maji ya mpito, iliyokuwa ikisimamia mradi wa maji hapa kijijini Ikombe, Ila amegundua kuwa hakukuwa na mawasiliano mazuri baina ya kamati ya mpito iliyokuwepo pamoja na kamati mpya iliyochaguliwa. Hivyo aliwataka wajumbe wa kamati ya mpito kutoa ushirikiano kwa kamati ya sasa kwani tofauti zao zimeongelewa leo na kufikia muafaka baina pande zote mbili. 

Kwa kufanya hivyo aliwataka wajumbe wa kamati, kushirikiana ili kuufanya mradi wao wa maji kusonga mbele. Pamoja na hilo amewataka wafanyakazi wa RUWASA wilayani hapa kuwatembelea Mara kwa mara wanakamati hao ili kuzidi kutoa elimu juu ya uendeshaji wa mradi wa maji. 

Aidha akikabidhi cheti na kanuni za jumuia ya watumia maji Ikombe, amewataka wajumbe wa kamati kuzingatia muongozo na taratibu za matumizi ya fedha za serikali, Pia kuzingatia amani na utulivu katika kijiji cha Ikombe kwa wakati wote huu wa kampeni hadi uchaguzi Mkuu, kwani serikali haijalala na itamshughulikia yeyote atakaekuwa chanjo cha kuvuruga amani hapa kijijini. 

Nae aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya maji ya mpito ndungu Assa s. Mwanyamaki amesema, yeye amekuwa kiongozi kwa miaka 6, na amekuwa na ushirikiano mkubwa na wajumbe wenzake hadi kuufanya mradi huo kufikia siku ya leo. Hivyo anawaomba wanakamati mpya kuiga mfano wao na wapo tayari kushirikiana kwa lolote ili kuifanya mradi kuwa endelevu. 

Ndugu Nazareth P. Mgunda ambae ni mwenyekiti wa kitongoji cha Isumba kijijini Ikombe, ametoa shukrani zake za dhati kwa serikali kwa kuwaletea mradi wa maji safi na salama kwani kabla ya hapo, walikuwa wakitumia maji ya ziwa ambayo ni safi lakini si salama. 


Watalaam kutoka serikalini wakiwa katika boti kuelekea kutoa huduma kwa wananchi katika kijiji cha Ikombe. 

Habari na Mawasiliano 

Kyela. 

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa