• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mheshimiwa Josephine Keenja Manase Afanya Ukaguzi Katika Mradi Wa Kituo Cha Afya Njisi

Imewekwa Kwenye: February 23rd, 2023

 Mkuu wa wilaya ya Kyela, Mheshimiwa Josephine Keenja Manase amefanya ukaguzi katika mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Njisi kilichopo kata ya Njisi hapa wilayani tarehe 23/02/2023.

Katika ukaguzi wake Mheshimiwa manase ametoa pongezi kwa kamati ya Ujenzi kwa hatua nzuri walipofikia katika ujenzi wa mradi huo.

 Aidha Mheshimiwa mkuu wa wilaya amesema, lengo la kutembelea mradi huo ni kutaka kujihakikishia kama shughuli za ujenzi zinaendelea kama zilivyopangwa, Na kuitaka kamati hiyo kuto muangusha katika umaliziaji wa ujenzi wa mradi huo.

Hata hivyo Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ya Kyela, ametoa shukrani zake za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa shilingi milioni 500 katika mradi huo, Na imani yake ni kwamba, mradi ukiisha kwa wakati na kwa kiwango cha juu, Mhe. Rais anapata imani ya kutupa hela za kuanzisha miradi mingine katika wilaya yetu. 

Pamoja na hayo Mheshimiwa Manase amewataka kukamilisha kwa wakati eneo la chumba cha mionzi (X-ray) kwa kutengeneza njia (walk way) ili kiweze kuanza  kutoa huduma, kwani mitambo imeshafungwa katika chumba hicho.

Aidha Mheshimiwa ametoa shukrani kwa Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera kwa kuujali mradi huo na kuwapenda wananchi wa kata ya Njisi kwa kujitolea nguvu zao katika ujenzi wa mradi huo.

Mwisho Mheshimiwa Mkuu wa wilaya ameridhishwa na kasi kubwa ya umaliziaji wa jengo la mama na mtoto na kuwahimiza kamati ya ujenzi kuendelea na kasi ya usimamizi wa kazi hiyo ili kuukamilisha mradi kwa wakati.

Nae diwani wa kata hiyo Mheshimiwa Omary Mwijuma, amemuomba mkuu wa wilaya Mheshimiwa Manase, kuwakumbuka katika kuanza ujenzi wa nyumba za watumishi katika kituo hicho cha afya mara baada ya kukamilika kwa awamu ya ujenzi inayoendelea.

Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa