• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Naibu Waziri Wa Afya Maendeleo Ya Jamii Jinsia Wazee Na Watoto Afanya Ziara Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: October 9th, 2021

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jami Jinsia, Wazee na Watoto (MB), Mheshimiwa Mwanaid Ali Khamis, amefanya ziara tarehe 08/10/2021 hapa wilayani Kyela, na kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha afya unaotekelezwa katika kata ya Itunge.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Itunge, Mheshimiwa Naibu waziri (MB), amewaomba wananchi wa kata ya Itunge kuendelea kushirikiana na kudumisha umoja walionao, ili kukamilisha ujenzi wa kituo cha cha afya, ambacho wameanza kukijenga kwa kasi kubwa, na ujenzi huo uweze kukamilika kwa wakati.

Amesema; “Ujenzi wa kituo hiki cha afya si mali ya wanaitunge wanaokijenga sasa, bali kituo hiki ni urithi kwa jamii nzima na kizazi kijacho” pamoja na hayo Mheshimiwa Naibu Waziri (MB), amesema serikali inawapenda wananchi wake hivyo, atahakikisha kituo cha afya itunge kinakamilika kwa wakati na alichangia ujenzi huo kwa kutoa mifuko 15 ya saruji. Pia aliwaagiza viongozi kutoka ngazi ya halmashauri kusimamia ujenzi huo ili kuhakikisha fedha iliyotolewa na serikali inatumika kama ilivyopangwa.

Aidha Mheshimiwa Mwanaid Ali Khamis amewakumbusha na kuwahamasisha wananchi wa kata ya Itunge kuzidi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa UVIKO 19, kwa kuchanja kwani ugonjwa huu ni hatari sana kwa afya zetu, Pia aliwahakikishia wananchi wa Itunge kuwa, punde ujenzi wa kituo hicho utakapokamilika serikali italeta vifaa kwa ajili ya kutoa huduma za afya kituoni hapo.

Pamoja na hayo, Mheshimiwa Naibu Waziri aliwasisitiza wananchi kujitokeza na kutoa ushirikiano wa dhati katika zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika mwakani, ili kuhakikisha kila mwananchi anahesabiwa.

Nae Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail T. Mlawa aliahidi kuchangia shilingi 500,000/= kwa ujenzi wa kituo hicho cha afya, na kumuahidi mheshimiwa Naibu Waziri kusimamia ujenzi wa kituo hicho hadi kitakapokamilika. Pia alitoa shukrani zake za dhati kwa serikali ya Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania kwa kuzidi kuikumbuka wilaya ya Kyela kwa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aidha Mbunge wa jimbo la Kyela Mheshimiwa Ally M. Jumbe aliishukuru serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kusikiliza kilio chake dhidi ya uchache wa vituo vya afya Kyela, na sasa serikali inajenga vituo 2 vya afya Kyela. Pia alimshukuru Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mhe. Katule G. Kingamkono na Mkurugenzi Mtendaji ndugu Ezekieli H. Magehema, kwa kubali kupeleka fedha kwa ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Ngonga na kata ya Itunge.

Mwisho Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Mwanaidi Ali Khamis (MB), aliweza kutembelea kikundi cha SHFA,kikundi kinachojishughulisha na utoaji wa elimu ya makuzi na malezi kwa watoto katika kata ya Mwanganyanga. Kikundi cha kilimo bidii cha wanawake katika kata ya Makwale, ili kujionea na kujifunza jinsi wanavyofanya kazi zao. 

kikundi cha wanawake "Kilimo Bidii" wakimkabidhi  Mheshimiwa Mwanaidi Ali Khamis Naibu Waziri(MB) mafuta ya mawese kama ishara ya konyesha sehemu yao ya utendaji wa kazi

Kikundi cha "SHFA" kikitoa burudani murua mbele ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO AONGOZA MCHAKATO WAKUMPATA MAKAMU MWENYEKITI WA MAMLAKA YA MJI MDOGO NA WENYEVITI WA KAMATI ZA KUDUMU

    October 01, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI ADV. FLORAH A. LUHALA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MAPATO YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    September 30, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA, MHE. JOSEPHINE MANASE, AMEKABIDHI HUNDI YA MFANO YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA SITA HAMSINI NA TATU LAKI SITA (653,600,000/=) KWA VIKUNDI 70 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    September 22, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA AFUNGA MAONESHO YA KUSINI INTERNATIONAL TRADE FAIR AND FESTIVAL YA MWAKA 2025

    September 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa