• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Serikali Imesaini Mkataba Wa Ujenzi Wa Barabara Hadharani Kyela

Imewekwa Kwenye: December 28th, 2022

WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema ujenzi wa barabara ya Ibanda-Kajunjumele,Kajunjumele-bandari ya Kiwira na Kajunjumele-bandari ya Itungi, wilayani Kyela, zenye urefu wa kilometa 32 kwa jumla, unatarajia kugharimu sh.bilioni 38.

Amesema barabara hizo zinazojengwa kwa kiwango cha lami, ni sehemu ya mtandao wa barabara muhimu za nchi inayounganisha mkoa wa Mbeya na mikoa ya Ruvuma na Njombe, kupitia Ziwa Nyasa katika bandari ya Itungi, Kiwira na Mbamba Bay.

Profesa Mbarawa aliyasema hayo jana tarehe 27/12/2022, mara baada ya kuushuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa barabara hizo, kati ya Mkurugenzi Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Rogatus Mativila na Meneja wa kampuni ya AVM-Dillingham International Inc., Mhandisi Umit Necat Pal. Mkataba uliosainiwa hadharani huku wananchi waliohudhuria katika hfla hiyo wakishuhudia. Na kwa mara ya kwanza Kyela imeandika historia ya uanzishwaji wa kusainisha mikataba ya serikali mbele ya wananchi.

Alisema barabara hiyo itakapokamilika itachochea shughuli za kiuchumi, kama vile usafirishaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo Kokoa, makaa ya mawe, mazao mbalimbali ya chakula na biashara, mazao ya misitu, uvuvi na shughuli za kijamii kwa ujumla.

“Leo tumeshuhudia muda mfupi uliopita, utiaji saini wa mkataba wa kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, barabara ya Ibanda-Kajunjumele yenye urefu wa kilometa 22, Kajunjumele-Kiwira Port yenye urefu wa kilometa 6 na Kajunjumele-Itungi yenye urefu wa kilometa 4” alisema Profesa Mbarawa.

Aliongeza barabara zote jumla zina urefu wa kilometa 32, na ujenzi wake utafanyika kwa kutumia fedha za ndani kwa asilimia 100.

Alisema ujenzi utakapokamilika, utarahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na za kijamii, kwa wananchi waioshio maeneo ya wilaya ya Kyela, Rungwe, Ruvuma na Njombe na inatarajiwa kuwa shughuli za kiuchumi za wananchi wanaoishi kandokando ya Ziwa Nyasa zitaimarika zaidi.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (sekta ya ujenzi), Mhandisi Godfrey Kasekenya, alisema Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, sasa ameamua kuifungua Tanzania, na ameamua kuifungua wilaya ya Kyela, mkoa wa Mbeya na mikoa yote ya nyanda za Juu Kusini.

“Rais Dk.Samia anataka ikiwezekana mtu akishusha mizigo yake bandari ya Mtwara, aje Tunduru, aje Songea, Mbinga, Mbamba Bay, lakini avuke na meli aje bandari za Kiwira ama ile ya Itungi wilayani Kyela, ataweza akaamua kwenda Kasumulu, anaweza akaamua kwenda wilayani Ileje, kwa maana ya Isongele kwenda nchini Malawi” alisema.

Aliongeza ama anaweza kwenda Tunduma-Sumbawanga hadi Kigoma, na hadi sasa kipande kitakachokuwa kimebaki cha vumbi ni kutoka Kasumulu hadi Isongele wilyani Ileje, kwa barabara yote lakini kwa kuanzia Tunduma kwenda maeneo mengine, wakandarasi wapo kazini.

Mkuu wa mkoa Mbeya, Juma Homera, alisema kwa utashi wake Rais Dk.Samia, anahakikisha kwamba mkoa huo unaletewa miradi kama kawaida na hususani katika wilaya hiyo ya Kyela, kwa lengo la kuufungua mpaka wa Kasumulu unaozitenganisha nchi za Tanzania, Malawi pamoja na mikoa mingine miwili (Njombe na Ruvuma).

“Tunamshukuru sana Rais Dk.Samia, ambaye amepanga kujenga barabara hii, na leo hii tunashuhudia utiaji saini wa mkataba kwa mara ya kwanza, unafanyika hadharani …” alisema Homera.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Rogatus Mativila, alisema barabara hiyo yenye jumla ya urefu wa kilometa 32, itajengwa kwa kiwango cha lami na mradi wa ujenzi wa barabara hizo ni moja ya mikakati ya serikali kuharakisha maendeleo ya nchi.


Matangazo

  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Tangazo La Mkopo February 14, 2023
  • Nafasi Za Kazi Tangazo Jipya January 01, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

    March 21, 2023
  • Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Kyela Afanya Kikao Kazi Na Watumishi Ili Kusikiliza Kero Zao

    March 17, 2023
  • Kamati Ya Siasa Ya Mkoa Wa Mbeya Imetembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Wilayani Kyela

    March 11, 2023
  • Maadhimisho Ya Siku Ya Mwanamke Yafana Wilayani Kyela

    March 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa