• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Serikali Yagawa Misaada Kwa Wahanga Wa Mafuriko Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: May 12th, 2022

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Juma Homera akizungumza na wananchi wa kata ya Katumbasongwe wakati wa kukabidhi misaada kwa wahanga wa mafuriko Kyela.

Wananchi wa kata ya katumbasongwe wakiwa wanamsikiliza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Homera amefanya ziara ya kuwatembelea na kuwapa pole wananchi wa kata ya Katumbasongwe kwa niaba ya wananchi wote wa wilaya ya kyela, walioathirika na mafuriko, yalitokea wilayani hapa usiku wa kuamkia tarehe 27.4.2022 hadi 28.4.2022 huku katumba songwe ikiwa ni miongoni mwa kata 17 zilikumbwa na mafuriko hayo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa misaada hiyo Mheshimiwa Homera ametoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ofisi ya waziri Mkuu TAMISEMI,Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kyela pamoja na Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Kyela kwa juhudi kubwa wanazozifanya za kuwasidia wananchi wa Kyela.

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amewaeleza wananchi hao kuwa, misaada iliyotolewa ni magodoro, mablanketi sukari na mafuta ya kupikia, na amesema misaada hiyo sio ya Katumbasongwe pekee, bali ya wananchi wote walioathiriwa na mafuriko, lakini pia amesema, ili kunusuru mafuriko ya mara kwa mara, seriklai kwa kushirikiana na nchi jirani ya Malawi  ina mpango wa kujenga bwawa kubwa ili kuweza kuwanusuru wananchi na mafuriko.

Aidha ametoa onyo kwa kamati ya maafa kuhakikisha kuwa hakuna upotevu wowote unaojitokeza kwenye misaada inayotelewa, Na kuwaomba viongozi wa kata, vijiji, vitongoji wagawe vitu hivyo kwa haki na sio kwa upendeleo ndani ya siku 2. Vilevile amewahidi wananchi wa kyela kuwa ujenzi wa madaraja utaanza hivi karibuni ili kurejesha mawailiano ya kata na kata.

Nae Mheshimiwa mkuu wa wilaya ya Kyela ASCP Ismail Mlawa amemueleza Mheshimiwa mkuu wa mkoa kuwa atasimamia vyema ugawaji wa misaada iliyotolewa, na kuwahidi wananchi kuwa, watu wote walioathirika na mafuriko na kuandikishwa watapatiwa msaada huo, Aidha amesema wakazi 46 wa kitongoji cha lugome kata ya Mwaya kwa hiari yao wameiandikia Ofisi ya Mheshiwa mkuu wa wilaya kuomba kuhamishiwa katika mazingira salama.

Pamoja na hayo Mkuregenzi mtendaji wa Halmashauri ya  wilaya ya Kyela, ambae ndie mwenyekiti wa kamati ya maafa wilaya Ndugu Ezekiel Magehema amesema jumla ya kaya 284 zimeathiriwa zaidi na mafuriko kwani nyumba zao zilibomoka kabisa na jumla ya watu 1,193 ikiwa wanaume ni 447 na wananwake 746 wameathiriwa sana.

 Aidha amesema nyumba 249 zimepata athari ndogo ndogo  kama kupata nyufa huku mashamba ya mpunga jumla ya hekta 10,616 zilizama na maji, pia mifugo yaani ng’ombe 101, nguruwe 200 na kuku 2,061 wote walisombwa na maji.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela (katikati) akiwa anamsikiliza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati wa ugawaji wa misaada kwa wahanga wa mafuriko Kyela.

Mathalani athari kubwa ya miundombinu kama barabara madaraja na baadhi ya shule zilingiliwa na maji na kulazimika kufungwa kwa muda mpaka maji yalipopungua na kupelekea jumla ya shule 27 za msingi na shule 5 za sekondari kufungwa kwa muda.

Madaraja ya waenda kwa miguu katika mto kiwira yameharibiwa kabisa na mafuriko, mfano daraja la Ibungu na daraja la Mwalisi ambayo yatahitaji matengenezo.

Magehema amesema kuwa kamati ya maaafa imebaini kuwa mahitaji ya kiutu yanayohitajika Zaidi ni kama chakula, magodoro, mashuka, blaketi, neti za mbu na dawa za kutibu maji ya kunywa.

Nae Mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Kyela ndugu Ally Jumbe Kinanasi amewaambia wananchi kuwa, serikali ya awamu ya sita inaendelea kufanya juhudi mbalimbali ili kuboresha miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko na kuwataka wawe na imani na serikali yao.

Mwisho baadhi ya wananchi walitoa shukurani zao kwa niaba ya wananchi wengine kwa KUishukuru Serikali ya awamu ya sita, kwa kuwajali na kuwasaidia wananchi hao katika kipindi wanachopitia baada ya mafuriko kutokea.

 

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAWAPUNGUZIA WANANCHI ADHA YA ELIMU KWA KUJENGA SHULE KARIBU YAO

    June 27, 2025
  • MAPATO YA NDANI YAIWEZESHA KYELA KUNUNUA MTAMBO WA KISASA WA KUTENGENEZEA BARABARA

    June 22, 2025
  • MKUU WA MKOA MBEYA MHE. DKT. JUMA ZUBERI HOMERA AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA KWA KUFIKISHA BILIONI 8.7 SAWA NA ASILIMIA 125% KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO

    June 17, 2025
  • MAADHIMISHO YA MTOTO WA AFRIKA YAFANA WILAYANI KYELA

    June 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa