• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Taasisi Ya Tanzania Interfaith Partnership (TIP) Yatoa Mafunzo Ya Kuzuia Ugonjwa Wa Kipindupindu Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: March 21st, 2023

Shirika lisilokuwa la kiserikali la Tanzania Interfaith Partnership (TIP) limefanya mafunzo ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Kipindupindu leo tarehe 20/03/2023, mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela.  

Mafunzo hayo yameshirikisha viongozi wa dini, walimu wanaofanya kazi katika shule za msingi na sekondari ambazo zipo katika maeneo ya mpakani baina ya Tanzania na Malawi. Ikiwa na lengo kubwa la kuwajengea uwezo wawezeshwaji hao ili waweze kwenda kutoa elimu katika maeneo wanayotoka hususani katika maeneo ya Makanisa, misikiti na shule zilizopo maeneo ya mpakani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuu wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Wilaya Dr. Saumu Kumbisaga amesema;

Anawashukuru wadau wa Tanzania Interfaith Partnership (TIP) kwa kuja kutoa elimu ya kujikinga na  maambukizi ya ugonjwa wa  kipindupindu, ugonjwa unaosumbua nchi ya jirani kwa sasa, kwani hii itakuwa ni mwanzo wa kutoa elimu kwa makundi makubwa kwa kupitia misikiti, shule pamoja na makanisa.

Hata hivyo amesema, anaamini timu yote inayopewa mafunzo leo, itakuwa ni timu yake ambayo atatembea nayo katika kutoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huu wa kipindupindu ikiwa ni pamoja na magonjwa ya mlipuko kama korona.

"Ni vizuri sisi ambao tunapata elimu hii kuendelea kutoa elimu kwa wenzetu, elimu ya  kuto fanya mikutano inayoshirikisha watu wengi na isiyokuwa ya lazima, kwani magonjwa ni mengi ikiwemo hata ugonjwa wa korona." Amesema  Dr. Kumbisaga.

Aidha Dr. Kumbisaga amesema lengo la kushirikisha makundi haya, ni kuifanya Kyela iweze kufikiwa na elimu hii kwa haraka, na kuifanya Kyela salama na Tanzania kwa ujumla wake.

"Timu hii baada ya mafunzo tunawaomba mhakikishe mnakua mabalozi wa kusisitiza wazazi kupeleka watoto kupata chanjo mbalimbali kwani magonjwa mengine ya milipuko kama, polio, surua yanazuilika kwa chanjo". Amesema Dr. Saumu Kumbisaga.

Mwisho aliwatakia mafunzo mema washiriki wote wa mafunzo hayo.

Shirika la Tanzania Interfaith Partnership(TIP) ni Shirika lisilokuwa la Kiserikali linaloundwa na Taasisi Kuu nne za kidini Tanzania yaani, Jumuia Ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza La Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), BARAZA la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Na ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar ( MoZ), lengo la shirika au taasisi hii ni kutoa huduma kwa jamii, katika masuala ya Afya, Ustawi wa jamii na ulinzi wa watoto, kupitia miundo ya Taasisi za kidini.

Mwisho.

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili April 18, 2023
  • Ajira Ajira Ajira April 18, 2023
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Matokeo Kidato Cha Nne Mwaka 2022 January 29, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Awataka Wananchi Kata Ya Makwale Kuishi Kwa Upendo

    May 19, 2023
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Awataka Wananchi Kata Ya Makwale Kuishi Kwa Upendo

    May 19, 2023
  • DC Awataka TANESCO Kutoa Elimu Ya Matumizi Ya Simu Kuunganishwa Na Huduma Ya Umeme

    May 16, 2023
  • Wauguzi Watakiwa Kuwa Na Lugha Rafiki Kwa Wagonjwa

    May 13, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0756944794

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa