• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TMDA Nyanda Za Juu Kusini Yatoa Elimu Ya Matumizi Sahihi Ya Dawa Kwa Wananchi Wilayani Kyela

Imewekwa Kwenye: November 21st, 2023

Katika kufanya maadhimisho ya wiki ya kuongeza uelewa kwa jamii juu ya kupambana na usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya matumizi yasiyo sahihi ya dawa, maadhimisho yanayoendelea kufanyika kuanzia tarehe 18/11/2023 hadi tarehe 24/11/2023, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Afya TMDA kwa kushirikiana na wadau wengine wametoa elimu ya usugu wa vimelea dhidi ya matumizi  ya dawa katika maeneo mbalimbali hapa wilayani Kyela.

Akitoa elimu kwa wafanyabishara katika kata ya Mababu kijiji cha Ngyeke, Jofrey Kikoti mkaguzi wa dawa TMDA nyanda za juu kusini amesema,

Usugu wa vimelea ni hali ya vimelea vya magonjwa kustahamili nguvu ya dawa iliyokusudiwa kuuwa vimelea, hasa vimelea vinavyosababisha magonjwa kwa binadamu, mifugo, samaki, mimea pamoja na bacteria, fangasi, virusi na protozoa.

Aidha bwana Kikoti ameeleza kwamba, mambo yanayosababisha  usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, ni pamoja na mgonjwa kupewa au kutumia  kiasi kidogo au kikubwa cha dawa zaidi ya  ilivyokusudiwa.

Pia mgonjwa kutomaliza dozi ya dawa kama ilivyoelekezwa wakati wa matibabu, tabia ya mgonjwa au mfugaji kununua au kutumia dawa bila kupata ushauri wa wataalamu, matumizi ya dawa hususani antibaotiki kwenye chakula cha mifugo yasiyozingatia ushauri wa kitaalam kwa ajili ya kunenepesha au kuharakisha ukuaji wa mfugo.

Vile vile amesema, matumizi holela ya dawa mfano, kwenye kilimo cha bustani, kutupa dawa au mabaki ya dawa na vifungashio bila kufuata utaratibu.

Pamoja na hayo ndugu Kikoti ametoa njia mbalimbali za kukabiliana na matumizi holela ya dawa ikiwemo, kuepuka tabia ya kutibu mifugo mwenyewe bila kuzingatia ushauri wa wataalamu wa mifugo, ameshauri njia  bora za ufugaji hasa unaozingatia chakula na matumizi bora ya chanjo.

Aidha ndugu Kikoti, amewafundisha wananchi kupunguza matumizi ya dawa yoyote kwa ajili ya kukinga magonjwa au kunenepesha mifugo bila ushauri kutoka kwa mtaalamu wa dawa.

Mwisho amewataka wananchi kuepuka matumizi holela ya dawa ili kuokoa maisha. Elimu hiyo itaendelea kutolewa katika maeneo mengine hadi siku ya kilele cha maadhimisho tarehe 24/11/2023.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa