• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waheshimiwa Madiwani Wilaya Ya Kyela Watembelea Na Kukagua Miradi Ya Maendeleo

Imewekwa Kwenye: July 28th, 2023

Mheshimiwa Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Katule G. Kingamkono(kushoto) akizungumza machache na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Bi. Florah A. Luhala (katikati) walipokuwa wakikagua miradi ya maendeleo.

Waheshimiwa Madiwani wilaya ya Kyela wametembelea na kukagua miradi ya maendeleo, ikiwa ni utekelezaji wa ziara za kutembelea na kukagua miradi kwa kipindi cha robo ya nne kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 27 hadi 28/07/2023, ikijumuisha Kamati ya Elimu na Afya, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Mkurugenzi Mtendaji Bi. Florah A. Luhala akiwa na wataalamu kutoka Idara mbalimbali za Halmashauri.

Waheshimiwa Madiwani na wataalamu wametembelea Mradi wa ukarabati wa kituo cha walimu (TRC) katika shule ya msingi Ikolo, mradi wenye thamani ya shilingi 22,000,000, Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa katika shule ya msingi Ipyana mradi wenye thamani ya shilingi 40,000,000, Ujenzi wa shule Mpya kata ya Njisi yenye thamani ya shilingi 538,500,000, Ukaguzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 112,500,000 katika zahanati ya  Kilasilo.

Baadhi ya vifaa tiba vilivyonunuliwa na kukaguliwa katika zahanati ya kilasilo kata ya Ikimba.

Pamoja na miradi hiyo, Miradi mingine iliyotembelewa na kaguliwa ni mradi wa taa za barabarani kata ya Bondeni njia panda Kapwili, Ukaguzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 112,500,000, Kikundi cha vijana waliokopeshwa fedha kupitia mfuko wa kusaidia wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, na kununua bodaboda katika kata ya Ibanda, pamoja na ujenzi wa shule mpya ya msingi katika kata ya Ikimba.

Moja ya jengo la madarasa katika shule mpya ya msingi inayojengwa katika kata ya Ikimba.

Miradi yote iliyotembelewa na kukaguliwa imeridhiwa na waheshimiwa madiwani ikiwa ni pamoja na kutoa pongezi zao za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuleta fedha nyingi zinazotekeleza miradi mbalimbali katika wilaya ya Kyela.

Aidha waheshimiwa madiwani wametoa maagizo ikiwemo agizo la umaliziaji wa miradi ya maendeleo kwa ubora na kuzingatia muda uliyopangwa.

Mradi wa taa za barabarani katika eneo la njia panda Kapwili kata ya Bondeni.

Hayo yote yamepokelewa na timu nzima ya wataalamu wa halmashauri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Bi. Florah A. Luhala, na kuwaahidi waheshimiwa kuyatekeleza kwa wakati maagizo na ushauri uliotolewa katika ziara hiyo.

Ziara hiyo itakamilishwa tarehe 31/07/2023 mara baada ya kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kutembelea miradi.

Waheshimiwa Madiwani wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa