• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wakazi Wa Kata Ya Itope Waomba Kusambaziwa Umeme Katika Vitongoji Vyote

Imewekwa Kwenye: May 13th, 2023

Wakazi wa kata ya Itope wilayani Kyela, wamemuomba Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Josephine K. Manase, kuwasaidia katika kumuomba Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili aweze kuwasambazia umeme katika vitongoji vyote vya kata yao.

Maombi hayo yametolewa na wananchi wa kata hiyo tarehe 10/05/2023, wakati Mhe. Mkuu wa wilaya alipowatembelea wananchi hao, kwa lengo la kufanya mkutano wa kusikiliza kero.

Mkuu wa wilaya ya Kyela (katikati) akiwa ametembelea msingi wa mradi wa ujenzi wa zahanati katika kata ya Itope kabla ya kufanya mkutano wa hadhara.

Akizungumza na wakazi wa kata ya Itope Mkuu wa wilaya ya Kyela, amewatoa hofu wakazi wa kata ya Itope kuwa Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesikia kilio cha wananchi wa kipato cha chini hivyo ameongeza awamu nyingine ya kusambaza umeme wa REA.

Ambapo tathmini ya zoezi hilo inafanyika kwa maeneo yote yanayostahili kusambaziwa umeme huo, Ikiwemo kata ya Itope, hivyo wananchi wajipange katika kuingiza umeme mara baada ya mradi huo kuwafikia.

Kuhusiana na ulipaji wa fidia katika mradi wa ujenzi wa  barabara ya Ibanda hadi bandari ya Kiwira na Kiwira Itungi port Mhe. Josephine amesema, fidia zote zitalipwa hakuna mwananchi atakae achwa bila kulipwa, kwa sasa Serikali inaendelea na mchakato wa maandalizi ya malipo ya kila mwananchi anaestahili kulipwa fidia.

Kuhusiana na uvumi wa mborea za ruzuku kutokuwa na ubora na kupelekea kutokea kwa magonjwa katika zao la mpunga na migomba, Mhe. Mkuu wa wilaya amewatoa hofu wakazi wa kata ya Itope kwamba, Hakuna mbolea iliyochakachuliwa kwani serikali imejiridhisha na ubora wake, Pia serikali ni sikivu na itazidi kufanya uchunguzi wa magonjwa yaliyojitokeza katika zao la Mpunga na Migomba.

Aidha amewapongeza wakazi wa kata ya Itope kwa kuomba waanzishiwe soko katika kata yao, kwani maeneo wanayo yakutosha. Ambapo Suala hilo lilichukuliwa na Mheshimiwa Mkuu wa wilaya na kuwaahidi anakwenda kulifanyia kazi.

Pia alimuagiza mtendaji wa kata kuhakikisha vitongoji vyote vimesomewa taarifa ya mapato na matumizi ndani ya wiki mbili, ili kutoa haki ya mwananchi kujua mapato na matumizi ya fedha zote zinazoingia na kuchangwa ndani ya kata yao.

Mheshimiwa Mkuu wa wilaya Mhe. Josephine K. Manase ameendelea na ziara zake za kusikiliza kero kutoka kwa wananchi, tarehe 12/05/2023 aliweza kufika na kufanya mkutano wa hadhara katika kata ya Ndobo kijiji cha Isuba, na kusikiliza kero kutoka kwa wananchi wa Ndobo na baadhi ya kero zilijibiwa na nyingine zilichukuliwa kwa utekekezaji.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • DED KYELA AFANYA KIKAO NA WATENDAJI KATA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI KAZI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA

    April 10, 2025
  • DC KYELA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KUANZIA JULAI HADI DESEMBA 2024

    March 29, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YAPONGEZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KYELA

    March 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa