• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

Imewekwa Kwenye: May 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe. Josphine Manase amewataka wauguzi wote Wilayani Kyela kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na uzalendo, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda miiko na maadili ya taaluma ya uuguzi ili kuhakikisha huduma bora kwa wananchi.

Akizungumza leo Mei 17, 2025 katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika Kiwilaya  Katika Hospitali ya Matema, Mhe. Manase amewaasa wauguzi kuendelea kuwa na nidhamu ya kazi, kuheshimu wateja wao, na kuhakikisha wanatoa huduma kwa huruma, upendo na ufanisi bila kujali changamoto zilizopo katika mazingira yao ya kazi.

Mhe.Manase Amefafanua kuwa Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Mama mchapakazi Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya ikiwemo ununuzi wa Vifaa tiba vya Kisasa na Majengo Bora hivyo  bila ya kuwepo kwa  huduma nzuri na bora kutoka kwa watoa huduma za afya, na hasa Wauguzi, uwekezaji huu hautakua na tija kwa Wananchi.

Hatahivyo Mhe. Manase amewaasa Wauguzi Wilayani Kyela kutumia Mfumo wa Pepmis kujaza taarifa zao zinazotakiwa ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa pindi unapofika muda wakupanda Madaraja kazini.

Vilevile Mkuu wa Wilaya amewataka Wauguzi hao kuendelea kutoa Elimu bila kuchoka Kwa jamii dhidi ya Mila potofu hasa kwa wakina Mama wajawazito waache kutumia Mitishamba wanayoiamini kuwa inawarahisishia kujifungua kwa urasi bila kufika katika Vituo vya kutolea huduma za afya badala yake watumiaji wa dawa hizo za kienyeji hupata matazo makubwa wakati wa kujifungua.

Aidha, Wauguzi hao walitumia fursa hiyo kuhuisha Uuguzi wao kwa kula kiapo upya na kuwasha mishumaa ikiwa ni ishara ya kuendelea kumuenzi muasisi wa kada ya Uuguzi Bi. Florence Nightingale

Sanjari na hayo Wauguzi hao walipata wasaa wa kuwasilisha Zawadi yao kwa Mkuu wa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Kyela Ndg. Saumu Seif Kumbisaga ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kujali na kuwathamini watoa huduma za Afya Wilayani Kyela

Ikumbukwe kuwa Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani hufanyika kila mwaka Mei 12 ili kutambua mchango mkubwa wa wauguzi katika sekta ya afya duniani kote.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAUGUZI WILAYANI KYELA WAADHIMISHA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI KATIKA HOSPITALI YA MATEMA

    May 16, 2025
  • KAMATI YA UCHUMI, UJENZI NA MAZINGIRA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA WILAYANI KYELA

    May 15, 2025
  • KAMATI YA SIASA MKOA YAPONGEZA UTEKELEZWAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI KYELA

    May 14, 2025
  • WALIMU WAKUU,WALIMU WA MANUNUZI, WAKUU WA SHULE,WATENDAJI WA KATA NA WA VIJIJI WAPIGWA MSASA MFUMO WA MANUNUZI (NEST)

    April 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa