• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wilaya Ya Kyela Yagawa Vyandarua Kwa Wanafunzi Wa Shule Za Msingi

Imewekwa Kwenye: November 20th, 2023

Katibu Tawala wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Bi. Sabrina Humoud Ruhwey amezindua zoezi la Ugawaji wa Vyandarua katika shule za msingi wilayani Kyela, Zoezi hilo limefanyika leo tarehe 20/11/2023 katika shule ya msingi Kyela.

Akizindua zoezi hilo, Bi. Sabrina Humoud Ruhwey amewataka walimu wa shule ya Msingi Kyela  kuhakikisha Watoto wote wa shule hiyo wanapata vyandarua, kama itakavyofanyika kwa watoto wa shule za msingi kuanzia darasa la kwanza mpaka darasa la 6.

Pamoja na hayo, Bi. Sabrina Ruhwey  amesema wanagawa vyandarua kwa lengo la kupambana na Malaria wilayani Kyela, pia amewataka wazazi wa kuhakikisha wanatumia vyandarua hivyo kwa matumizi sahihi.  Na si kwa shughuli nyingine za kijamii kama vile uvuvi wa samaki, kuweka uzio wa Bustani au kwa ufugaji wa kuku kwani kwa kufanya hivyo, kutadhoofisha vita dhidi ya Malaria.

Hata hivyo Bi. Sabrina Humoud amewatoa hofu wazazi kuwa vyandarua hivyo ni salama kabisa kwa binadamu, na havina madhara yeyote ya Kiafya kwa binadamu.

"kama watu wengine wenye dhana potofu wasemavyo kuhusu vyandarua hivyo kuwa vinapunguza nguvu za uzazi kitu ambacho hakina ukweli wowote kwani vyandarua hivyo vimepimwa na wataalamu wa afya kabla havijaruhusiwa kuingia nchini na kuanza kugawiwa" amesema Bi. Sabrina

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kyela ndg. Florah A. Luhala amewakumbusha wazazi kuchangia pesa ya chakula ili watoto waweze kupata chakula shuleni.

Bi. Florah Luhala ameongeza kuwa Siyo jambo zuri kwa watoto wachache kupata chakula na wengine kukosa chakula, kwa kuwa hawajachangia pesa ya chakula, kwani kufanya hivyo ni kunatengeneza chuki na utengano baina ya watoto.

Vilevile Bi. Florah Luhala amesema watoto wakipata chakula wote kwa pamoja shuleni kuna tengeneza Upendo na  Mshikamano, jambo ambalo hupelekea watoto Kusaidiana katika masomo na kurahisisha ufaulu mashuleni.

"Haileti picha nzuri watoto wengine wanakula wakati watoto wengine wamekaa pembeni wakiangalia wenzao wakila eti kwasababu hawajachangia, unaweza ukaona ni jambo la kawaida lakini siyo la kawaida kwa watoto, tunawaharibu ufahamu wao" Amesema Bi. Florah

Aidha Bi. Florah Luhala amehitimisha kwa kuwataka wazazi kuzingatia malengo ya vyandarua vilivyogawiwa na amewaomba wazazi wakavitumie kama ilivyopangwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA December 01, 2022
  • Matokeo Kidato Cha Nne Mwaka 2022 January 29, 2023
  • Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Kati 2020 June 17, 2020
  • Orodha Ya Majina Ya Walioteuliwa Kuwa Wasimamizi Na Makarani Waongozaji Katika Uchaguzi Mkuu October 28th 2020 October 19, 2020
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Miti 70,000 Yapandwa Katika Maadhimisho Ya Miaka 62 Ya Uhuru Wa Tanzania Bara Wilayani Kyela

    December 08, 2023
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mhe. Josephine Manase Azindua Zoezi La Ugawaji Wa Vitambulisho Vya Uraia Wilayani Kyela

    December 08, 2023
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mhe. Josephine Manase Azindua Zoezi La Ugawaji Wa Vitambulisho Vya Uraia Wilayani Kyela

    December 08, 2023
  • Mkuu Wa Wilaya Ya Kyela Mhe. Josephine Manase Azindua Zoezi La Ugawaji Wa Vitambulisho Vya Uraia Wilayani Kyela

    December 08, 2023
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA UJENZI WA MADARASA
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa