• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Kyela District Council
Kyela District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Fedha
      • Huduma za Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • mifugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Biashara na Viwanda
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi
      • TEHAMA
  • Fursa Za uwekezaji
    • Vivutio vya Utali
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, uongozi na mipango
      • Ukimwi
      • Uchumi, ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
      • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamirika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wilaya Ya Kyela Yatekeleza Agizo La Mheshimiwa Waziri Mkuu Kwa Kupanda Na Kugawa Bure Miche Ya Kakao Kwa Wakulima

Imewekwa Kwenye: January 30th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa (Katikati) akiangalia moja ya kitalu cha miche ya Kakao kilichopo kata ya Ipinda wilayani Kyela.

Wilaya ya Kyela imetekeleza agizo la Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim  Majaliwa, agizo lililotolewa tarehe 03/08/2021, ambalo lilimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya kuhakikisha anazalisha miche ya kakao na kuigawa bure kwa wakulima wilayani hapa.

Akikabidhi miche hiyo kwa baadhi ya wakulima, Mkuu wa wilaya ya Kyela Mheshimiwa Ismail Mlawa mesema, amegawa miche ya kakao kwa wakulima huku akiamini miche hiyo imetokana na mbegu bora, "ukiwa na uchumi mzuri katika wilaya unakuwa na uhakika wakuwa na wananchi wenye maisha bora, Pia wanakuwa na uwezo wa kuwapeleka watoto wao shule, kupata chakula cha uhakika na kupata huduma za afya bora" alisema.
Aidha alisema hakuna sababu wanaKyela kukaa vijiweni kwa sababu Kyela imebarikiwa kuwa na ardhi yenye rutuba, hivyo wananchi hatutakiwi kubweteka yatupasa kufanya kazi. 

Pia aliwaomba chama kikuu cha ushirika Kyela (KYEKU), kuongeza jitihada za kuzalisha miche ya kakao ili kila mkulima aweze kupata miche hii mipya na kuachana na ile ya zamani iliyozeeka.

Nae mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa Katule G. Kingamkono amewaambia wakulima kwamba, kwa kupitia Baraza la Waheshimiwa Madiwani, wamejipanga kwa kupitia mapato ya ndani, kuanza kuwekeza nguvu katika kilimo hususani katika uzalishaji wa miche ya kakao na michikichi, hivyo wakulima wakae mkao wa kula.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kyela Mheshimiwa Katule G. Kingamkono akiongea na baadhi ya wakulima kabla ya zoezi la kuwakabidhi miche ya kakao katika kata ya Ipinda Kyela.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima ndugu Jackson Gelevasi amesema wakulima wanawaomba watalaam wa kilimo kuwapitia wakulima katika mashamba yao ili kuweza kuwapa ushauri kwa ajiri ya Kuboresha zao hilo.

Chama Cha Ushirika Kyela (KYEKU) kimezalisha miche 13,510 ya kakao ikiwa ni miche 3510 zaidi kwa ajiri ya kufisia miche iliyokufa na kuharibika.

Moja ya kitalu safi cha miche ya kakao kilichopo kata ya Ipinda Kyela, ambacho miche yake itagawiwa kwa wakulima.

Matangazo

  • ORODHA YA ASASI ZILIZOPATA KIBALI CHA UANGALIZI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MWAKA 2024/2025 June 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA USAILI September 27, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DED KYELA AWATAKA WASIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA KWENYE MIRADI

    July 29, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA KYELA Adv FLORAH A. LUHALA AONGOZA TIMU YA MENEJIMENT YA KAMATI YA ELIMU NA AFYA KUKAGUA MIRADI.

    July 28, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA KYELA ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    July 22, 2025
  • DC MANASE AWATAKA MAAFISA UGANI KUWATEMBELEA WAKULIMA NA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    July 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Tume ya Uchaguzi
Video Zingine

Viungo Vya Haraka

  • Mbeya Region Website

Viunganishi Linganifu

  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration & Local Government - PORALG
  • Public Service Recruitment Secretariat - (PSRS)
  • KYELA DISTRICT
  • KYELA DISTRICT COUNCIL

Idadi ya wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

wasiliana nasi

    Bomani Street

    Sanduku la Posta: P. O box 320 Kyela

    Simu ya Mezani: 025-2540035/7

    Simu ya Mkononi: 0713655466

    Barua pepe: ded@kyeladc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Kyela. Haki zote zimehifadhiwa